Idadi ya vifo kutokana na maambukizi ya virusi vya corona ulimwenguni yazidi kuongezeka.


Idadi ya vifo kutokana na mambukizi ya virusi vya corona ulimwenguni yazidi kuongezeka, watu 998 747 wamekwishafariki  kutokana na virusi vya corona.


Idadi ya vifo kutokana na maambukizi  ya virusi vya corona  imeonegezeka  ikilinganishwa  na ilivyokuwa hapo awali.


Watu  milioni  33,5 wameambukiwa virusi hivyo. 


Idadi ya watu walioruhusiwa kuondoka hospitali  imefikia watu  milioni  24.4.


Nchini Marekani, watu   209 177 wamekwishafariki kutokana na  maambukizi ya virusi vya corona huku watu   milioni 7 wakiripotiwa kuwa na maambukizi ya virusi hivyo.


New York ndio eneo ambalo limeathirika kwa kiasi kikubwa na maambukizi ya virusi hivyo.


Nchini Uingereza , watu  34 wamefariki kutokana na maambukizi ya covid-19 ndani ya masaa 24.


Kutokana na vifo hivyo , idadi ya watu ambao wamefariki kutokana  na maambukizi ya virusi hivyo imefikia watu  41 971.


Idadi ya watu walioambukiwa virusi hivyo imefikia watu   laki 6.


Nchini Italia, watu  17 wamefariki ndani ya masaa 24 kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.


Idadi ya watu ambao wamefariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona  imefikia watu  35 818.


Nchini Ufaransa,  watu  39 wamefariki  ndani ya masaa  24 kutokana na maambukizi ya virusi vya corona huku idadi ya watu  waliofariki ikitajwa kuwa watu  31 700.